| Chapter 2 |
1 |
Kwanza kabisa, basi naomba dua, sala, maombi na sala za shukrani zitolewe kwa Mungu kwa ajili ya watu wote, |
2 |
kwa ajili ya wafalme na wote wenye mamlaka, ili tupate kuishi maisha ya utulivu na amani pamoja na uchaji wa Mungu na mwenendo mwema. |
3 |
Jambo hili ni jema na lampendeza Mungu Mwokozi wetu, |
4 |
ambaye anataka watu wote waokolewe na wapate kuujua ukweli. |
5 |
Maana yuko Mungu mmoja, na pia yuko mmoja anayewapatanisha watu na Mungu, binadamu Kristo Yesu, |
6 |
ambaye alijitoa mwenyewe kuwakomboa watu wote. Huo ulikuwa uthibitisho, wakati ufaao ulipowadia. |
7 |
Kwa sababu hiyo mimi nilitumwa niwe mtume na mwalimu wa watu wa mataifa, niutangaze ujumbe wa imani na ukweli. Nasema ukweli; sisemi uongo! |
8 |
Basi, popote mnapokutana kufanya ibada nataka wanaume wasali, watu waliojitolea kweli na ambao wanaweza kuinua mikono yao wakisali bila hasira wala ubishi. |
9 |
Hali kadhalika, nawataka wanawake wawe wanyofu na wenye busara kuhusu mavazi yao; wavae sawasawa na si kwa urembo wa mitindo ya kusuka nywele, kujipamba kwa dhahabu, lulu au mavazi ya gharama kubwa, |
10 |
bali kwa matendo mema kama iwapasavyo wanawake wamchao Mungu. |
11 |
Wanawake wanapaswa kukaa kimya na kuwa wanyenyekevu wakati wa kujifunza. |
12 |
Mimi simruhusu mwanamke amfundishe au amtawale mwanamume; anapaswa kukaa kimya. |
13 |
Maana Adamu aliumbwa kwanza, halafu Hawa. |
14 |
Na wala si Adamu aliyedanganywa; bali mwanamke ndiye aliyedanganywa, akaivunja sheria ya Mungu. |
15 |
Hata hivyo, mwanamke ataokolewa kwa kupata watoto, kama akidumu katika imani, upendo, utakatifu na unyofu. |